BUSARA HUTUSAIDIA KUTENDA KWA MAKINI - GOLDGREENZ

"Mind is the greatest asset of all the time" ---Goldgreen

HEADLINE

http://onvictinitor.com/afu.php?zoneid=3013357

Wednesday, September 20, 2017

BUSARA HUTUSAIDIA KUTENDA KWA MAKINI



Usipotenda kwa umakini unaweza kujichukia na mambo mengi hayatoenda sawa. Kila mtu anahitaji mtu mwenye nguvu zaidi yake amnyanyue. Na mtu mwenye nguvu ni yule mwenye busara.
Kwasababu hata kama mtu ana nguvu kiasi gani kama hana busara atakuja kukamatika tu na asione njia ya kupita. Ni muhimu sana kukaa karibu na mtu mwenye hekima na kujifunza kutoka kwake.
Matatizo kila siku yanapiga hodi na yanahitaji hekima kuyatatua. Ni Muhimu sana kuwa na busara kwasababu ndio yenye kutusaidia kufanya maamuzi yaliyo bora katika maisha yetu. Itatusaidia kujenga familia zetu na hata taifa letu.
Pesa haiwezi kufanya hivyo. Haiwezi hata kidogo. Bali ukiwa na pesa na busara umebarikiwa kweli kweli. Jitupe chini na mshukuru Mungu ukiwa na hivyo vitu viwili vitakupatia Great Comfort. NO man can be Great without WISDOM. DRINK A CUP OF WISDOM
Kila tendo letu tunalofanya huunda kitu. Hii iwe kwa kujitambua au kutokujitambua. Lakini wale wanaotenda kwa kujitambua ndio wanaoendelea zaidi kuliko wale ambao hawatendi kwa kujitambua.
Kushindwa kufanya chaguzi bora ambazo zitakufanya usonge mbele ni udhaifu wa kiakili. Ndio maana kuna usemi unaosema kabla haujatenda kitu chochote fikiri kwakuwa huwezi kurudisha muda nyuma ukiisha tenda jambo na majuto ni mjukuu.

Kwahiyo binadamu anatakiwa kuwa makini katika fikra na matendo yake. Kutenda yaliyo sahihi na yenye faida sio tu kwake mwenyewe bali pia kwa jamii yake na taifa lake.

No comments:

Post a Comment