UMASIKINI WETU NI MATOKEO YA MATUMIZI MABOVU YA MUDA WETU - GOLDGREENZ

"Mind is the greatest asset of all the time" ---Goldgreen

HEADLINE

http://onvictinitor.com/afu.php?zoneid=3013357

Wednesday, September 20, 2017

UMASIKINI WETU NI MATOKEO YA MATUMIZI MABOVU YA MUDA WETU



Kwa mujibu wa sheria zetu muda rasmi wa kufanya kazi kama ulivyowekwa na sheria ni masaa nane yaani kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi alasiri na muda mwingne kuacha utumike kwa mambo mengine ikiwemo kupumzika n.k
Sasa chukua simple facts hizi kisha ufanye reflection naamini kuna kitu utajifunza, siku moja ya kibinaadamu ina masaa 24 lakini sheria zetu ambazo zimezaa utamaduni zinaelekeza kazi ifanyike kwa masaa 8 ambayo in fact n asilimia 33 tu ya muda wote kwa siku
Then wiki moja yenye siku 7 muda wa kazi kwa mujibu wa sheria tena ni siku 5 yaani jumatatu mpaka ijumaa ambapo kwa dhana ya masaa ni kwamba wiki moja yenye siku saba mara masaa ishirini na nne unapata kwamba wiki moja ina masaa 168 lakni muda wa kazi kwa siku tano za wiki kwa masaa nane kila siku n masaa 40 tu kwa wiki na kuacha masaa mengne 128 kwa mambo mengne nje ya kazi.
Chukua tena simple facts ambazo haziitaji uwe na PhD kung'amua ni kwamba mwezi mmoja una masaa 720 lkn masaa ya kazi ni 160 tu kwa maana ya siku 20 za kazi kwa mwezi ,na vivyo hvyo kwa mwaka wenye masaa 8640 muda wa kazi ni 22% yake yaani masaa 1,920.

Wakati wenzetu wanaanza kujikomboa katika minyororo ya kiuchumi iwe kwa level ya mtu mmoja mmoja au kwa level ya kitaifa suala la matumizi sahihi ya muda ilikuaga n kipaumbele chao cha kwanza kwa maana tukiwa na matumizi sahihi ya muda then yaambatane na utendaji kazi na ufanyaji kazi kwa bidii na maarifa basi kwa namna yoyote ile lazima tutapiga hatua.
Tatizo na mifumo yetu ni je kwa kuwa muda wa kazi uliopo kisheria unatupa muda mwingine mwingi wa kufanya mambo mengine sasa hiyo extra ordinary time tunaitumia productively?? Au ndio muda ambao tunatumia kwa ajili ya kukifyonza hata kile kilichovuna katika kazi iliyofanyika kwenye yale masaa 8 ya kazi?
Lakini je hata huo muda kidogo wa kazi tunafanya kweli kazi kizalendo,kwa welendi,juhudi na maarifa? Je tunafanya tukiwa na dhamira ya kujikomboa kweli?? Au ndio muda huo huo finyu wa kazi tunapachika na mengineyo nje na utashi na matarajio?



jibu lake ni simple kwamba tunachanganya majukumu katika muda uliochangamana na kazi na kufanya kazi katika muda uliochangamana na majukumu matokeo yake tunakosa vipaumbele kwa kuwa hatuna muda mzuri wala uzuri wa muda hatuujui.

No comments:

Post a Comment