TEKNOLOJIA ILIVYO KIRUSI CHA MAPENZI - GOLDGREENZ

"Mind is the greatest asset of all the time" ---Goldgreen

HEADLINE

http://onvictinitor.com/afu.php?zoneid=3013357

Wednesday, September 20, 2017

TEKNOLOJIA ILIVYO KIRUSI CHA MAPENZI


Tunapokubaliana na ukweli kuwa mitandao ya kijamii inarahisisha upatikanaji wa mapenzi, tukubaliane pia kuwa teknolojia imefanya mwenzi wako apatikane kiurahisi zaidi.
Tofauti na zamani kwamba ili mtu amfikie mke wa mtu inabidi avae ujasiri hasa, na kutumia njia za kijasusi ili kumpata, siku hizi urahisi ni mkubwa. Ukishamjua jina, unamfuata mtandaoni kisha mengine yanaendelea.
Mke wa mtu ukishapata namba yake ya simu, mambo mengine yanendelea, kuchati na kupigiana simu. Jamaa anaonesha kumjali mke wa mwenzake kuliko anavyomjali mkewe. Mwisho mwanamke naye anasaliti. Teknolojia imekuwa kirusi hatari.




Mke wa mtu anapost picha zenye kumuonesha anavyovutia. Mume hatokei kumsifu mke wake, matokeo yake wakora wanatokeza kumwaga pongezi, mwisho mwanamke anaona kumbe anapendwa nje kuliko ndani. Matokeo yake anatoa shukurani zake kwa upendo wa nje.
Mume wa mtu anapita mitanadao ya kijamii anaona warembo wa kila aina. Anatoa maoni kwenye picha zao au ana-like. Mwingine maoni na like zake anakwenda kutumbukiza inbox ya mrembo husika. Mrembo akiwa mwepesi naye anajibu na masuala mengine yanafuata.
Nyumba moja, mume anakuwa ‘bize’ kusifia wanawake wenye muonekano wa kimitindo, anamwaga pongezi “mtoto ana fugure namba nane”, mwingine anasifia makalio “mrembo mgongoni amejaliwa”, wakati huo mke wake naye yupo na picha ya kijana mwanamazoezi “mkaka handsome ana six-pack.” Mume kumfikia huyo wake wa namba nane ni rahisi, mke naye na kijana wake wa six-pack anamfikia kirahisi mno. Ni utaratibu huo ambao umekuwa ukisababisha mapenzi na ndoa viwe kwenye majaribu mazito ya uaminifu. Teknolojia inaziingiza ndoa nyingi kwenye chumba cha mtihani.
Lipo janga la makundi ya mitandao, mfano WhatsApp na Facebook Messenger, muunganiko ni mkubwa mno. Unaunganishwa kwenye kundi na watu ambao ulikuwa hufahamiani nao.

Katika kuchangia mada mbalimbali kwenye kundi, watu wanahama kutoka kwenye mijadala ya wazi, wanaanzisha mawasiliano ya faragha. Kwamba mtu ameona namba ya mtu kwenye kundi, anamtumia ujumbe inbox au anampigia simu. Mawasiliano yanaendelea mwisho wanafikishana kwenye mapenzi.

No comments:

Post a Comment