DARASA HURU KUHUSU NDOA NA HARUSI KWAKO MWANAUME MWENZANGU - GOLDGREENZ

"Mind is the greatest asset of all the time" ---Goldgreen

HEADLINE

http://onvictinitor.com/afu.php?zoneid=3013357

Wednesday, September 20, 2017

DARASA HURU KUHUSU NDOA NA HARUSI KWAKO MWANAUME MWENZANGU




Haijalishi ukubwa wa harusi uliyofanya kitu cha muhimu ni unachokwenda kukijenga baada ya harusi, baada ya watu wote kuondoka na kuwaacha peke yenu mwende nyumbani, mkaanzishe maisha yenu. hiko ndicho cha muhimu na ndicho kinachotakiwa kupewa umakini mkubwa. Usisahau hilo jua kwamba una kazi kubwa mbele yako, na usichukulie harusi kwa ukubwa usiostahili zaidi ya kile unachoenda kukijenga. "Familia"
Harusi ni ya siku moja, lakini unachokwenda kukijenga huenda kikaishi muda, zaidi ya uhai wako. Kwakuwa misingi utakayo wajengea watoto wako ndio misingi hiyo hiyo watakayo wajengea watoto wao. Ubora wa familia yako huenda ukawa pia ubora wa familia zao.
Inategemea ulivyolelewa na wewe utawalea hivyo hivyo. Kwahiyo kwa mwanamume hana haja ya kufurahia sana harusi bali kufikiri kazi iliyo mbele yake. Kulea watoto katika maadili na nidhamu.
Kulea watoto kama simba walio nyikani, ili wakabiliane na changamoto zote za duniani. Kwasababu maisha ya duniani sio rahisi sana yanahitaji busara kukabiliana nayo. Unawezaje kufanya harusi kubwa na kujenga baadae kisicho na thamani? Ewe kichwa cha familia?


No comments:

Post a Comment