ADUI AKISHINDWA MPANGO WAKE MBAYA UKILIPA KISASI HUTAFANIKIWA - GOLDGREENZ

"Mind is the greatest asset of all the time" ---Goldgreen

HEADLINE

http://onvictinitor.com/afu.php?zoneid=3013357

Wednesday, September 20, 2017

ADUI AKISHINDWA MPANGO WAKE MBAYA UKILIPA KISASI HUTAFANIKIWA




Kipindi mafunzo yamekolea na askari hao wakiwa wameshakamilika tayari kwa utekelezaji wa mauaji hayo, lilitolewa agizo la Serikali kuwa mpango wa Kikosi 684 umefutwa.
Sababu ya kufutwa mpango huo ni kufuatia maelewano ya kidiplomasia kati ya Korea Kusini na Kaskazini kufikia hatua nzuri. Kipindi hicho Kikosi 684 kilikuwa bado kipo Silmido.
Agosti 23, 1971, makomando wa Kikosi 684 waliua walinzi wao pamoja na wahudumu, wakavuka Bahari ya Njano (Yellow Sea), wakateka basi na kupanda kuelekea mji mkuu wa Korea Kusini, Seoul.
Safari yao ikawa kuelekea Ikulu ya Korea Kusini, Blue House ili kumuua aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Park Chung-hee.
Vikosi vya Jeshi la Korea, vilikizingira Kikosi 684, katika eneo la Daebang-dong, Dongjack-gu, Seoul. Askari 20 wa Kikosi 684 waliuawa na wengine kujiua eneo la tukio, wanne waliobaki walihukumiwa kifo na walinyongwa Machi 10, 1972.
Mpaka leo swali limebaki ni sababu gani Kikosi 684 walitaka kumuua Rais Chung-hee? Huo ndiyo uasi wa kijeshi ambao haujawahi kubainika sababu yake.
MATOKEO
Serikali ya Korea Kusini ilinyamaza, haikutoa taarifa yoyote kuhusu makomando wa Kikosi 684.
Mwaka 2006, Korea Kusini iliamua kuvunja mzizi wa fitina kwa kueleza bayana kilichotokea kuhusu Kikosi 684.
Baada ya taarifa hiyo, familia za makomando wa Kikosi 684 waliipeleka Serikali mahakamani na kushinda kesi.
Serikali iliagizwa kuzilipa fidia familia za makomando wa Kikosi 684 kwa sababu makomando hao walipewa mafunzo makali bila tahadhari yoyote. Walivurugikiwa akili na kujaribu kufanya shambulio. Serikali badala ya kuwaelewa kuwa hawakuwa sawa, wakawachukulia kama waasi.
NINI UNAPATA?
Korea Kusini waliingia gharama kubwa zaidi walipojaribu kulipa kisasi. Walipoteza makomando wote 31. Chupuchupu Rais wao auawe. Zaidi, waliingia gharama ya kuendesha kesi na kunyonga kisha kulipa fidia familia za marehemu wote 31.
Adui yako akishindwa mpango wake mbaya juu yako, shukuru Mungu ambaye amekunusuru. Usijione umemzuia kwa nguvu na maarifa yako.

Ukijiona jabali na kupanga kulipa kisasi, unakuwa unamkosea Mungu aliyekulinda.

No comments:

Post a Comment