KICHAA CHA NGONO - GOLDGREENZ

"Mind is the greatest asset of all the time" ---Goldgreen

HEADLINE

http://onvictinitor.com/afu.php?zoneid=3013357

Wednesday, September 20, 2017

KICHAA CHA NGONO




Kuna watu hufunga safari pamoja mpaka hotelini. Tena wanaweza kuingia ndani wakiwa wameshikana mikono, kukumbatia na hata kupigana mabusu. Ajabu ni kuwa wakishamaliza haja zao, kile kichaa chao cha ngono kinawapotea kwa muda. Wanaona aibu kutoka pamoja, wanaambiana “anza wewe kutoka.” Kichaa cha ngono hukata mshipa wa aibu.
Mwanaume kwenda kutembea na ndugu wa mkewe au hata mama mkwe wake, hicho kama siyo kichaa cha ngono ni nini? Mwanamke kutoka na shemeji zake au baba mkwe wake, hicho ni kiwango cha juu kabisa cha maradhi ya kichaa cha ngono.
Kwa kawaida kichaa cha ngono hufanya kazi yake iliyodhamiria. Kikikupanda kisha kikakutuma uwe unatongoza na kutembea na marafiki wa mkeo, hata ukiwa unaumwa upo kitandani hujigeuzi, wakija kukuona kwa heshima ya urafiki wao na mkeo, wewe utatumia kila hila mpaka uombe namba ya simu.
Kichaa cha ngono kikimtuma mke wa mtu kuwamaliza marafiki wa mume wake, atakuwa kimbelembele kuwajali marafiki zake utafikiri mtu kweli. Ukarimu mwingi, kumbe ule ukarimu wake tafsiri yake ni ngono. Ukishakijua kichaa cha ngono hakikusumbui.
Usiombe ukutane na mwanamke ambaye anaumwa kichaa cha ngono, anaweza kuzungukwa na wanaume 10 halafu wote hawajuani, kila mmoja anadhani yeye peke yake ndiye anakula. Anakuwa na mumewe ambaye anajulikana kisha marafiki tisa wa mumewe. Hao marafiki kila mmoja anaamini yeye ndiye anakula kwa siri nje ya mwenye mali. Kumbe wote pale wanakula.

Mwanamke anawapanga, stori za mezani kisha kwenye simu zinaendelea SMS: “Natamani baada ya kutoka hapa tukalale wote, sema tu jamaa hapa anabana.” Hiyo SMS anaituma kwa wanaume wote tisa kasoro mume wake, halafu kila mmoja anaamini katumiwa peke yake, kisha anajibu kwa madaha ya kuamini anapendwa: “Usijali baby, next time, you know I love you kuliko mume wako.” SMS hiyo ikajibiwa na wanaume wote tisa, mwanamke huyo roho kwatu kwa kujiona yeye ndiye mwanamke wa shoka anayeweza kuwaendesha wanaume 10 kwa wakati mmoja bila kujuana. Anawachanganya tu kama karanga za Saida Kalori. Ile hali ya mwanamke huyo kujiona mjanja kwa ukahaba anaofanya ndiyo matokeo ya kichaa cha ngono kukomaa.

No comments:

Post a Comment