MAMBO YA KUJUA KABLA YA KUMPATA MWENZI WAKO - GOLDGREENZ

"Mind is the greatest asset of all the time" ---Goldgreen

HEADLINE

http://onvictinitor.com/afu.php?zoneid=3013357

Wednesday, September 20, 2017

MAMBO YA KUJUA KABLA YA KUMPATA MWENZI WAKO




Unapopata mpenzi au tayari unamtambua kama mwenzi wa maisha yako kwa sababu tayari mpo kwenye ndoa, unapaswa kuzingatia kuwa binadamu wana historia tofauti za kimaisha.
Huyo mwenzi wako anaweza kuwa anatabasamu na wewe leo, lakini kabla ya kukutana na wewe, ametoka kulia machozi mengi mno. Baada ya kukutana na wewe anakuona faraja na kifutio cha machozi yake yote ya nyuma.
Unaweza usiwe ndani yake kujua ni kwa kiasi gani alikata tamaa ya maisha kabla ya kukutana na wewe. Hata hivyo, baada ya kukupata, ghafla anajiona yupo kwenye ulimwengu mpya wenye raha zenye kumsahaulisha kumbukumbu mbaya alizopitia.



Nakwambia huwezi kujua baada ya kukupata umemfanya ajae matumaini ya kiasi gani. Na huwezi kutambua ni kwa thamani kubwa kiasi gani anakuthamani baada ya yote magumu aliyopitia kabla yako.
Kwa vile huishi kwenye fikra zake hutaweza kutambua ni kwa kiasi gani wewe ndiye mantiki ya dunia yake. Jinsi anavyokuhitaji ni sawasawa na anavyoihitaji dunia. Sababu ni moja tu kwamba ametoka kwenye mengi yenye kumtesa kabla yako.





Anakuheshimu na unaona, anakupenda na huo upendo wake unauhisi kikamilifu. Wajibu wako unakuwa ni mmoja tu, kumpenda sawasawa na anavyokupenda au wewe zidisha. Mpe heshima sawasawa na anavyokuheshimu au mzidishie. Ukifanya hivyo, utamfanya azidi kuiona dunia imenyooka sana upande wake baada ya kukupata.
Ikiwa mwenzi wako anakuona wewe ni dunia yake, maana yake wewe pia ni kifo chake. Dunia isipokuwepo kuna maisha tena? Sasa basi, hakikisha upepo na imani yake kubwa kwake unavitunza na unampa uhakika kuwa yupo kwenye mapenzi salama.

Ukienda kinyume utamsababishia mauti mwenzako. Ukimtenda utamrejeshea kumbukumbu mbaya alizodhani amezifuta. Lazima utambue nafasi yako kwenye mapenzi na maisha yako yawe ulinzi tosha kwake.

No comments:

Post a Comment