KATIKA KILA TENDO, KUNA MATOKEO KUSUDIWA AU MATOKEO YALIYO KINYUME - GOLDGREENZ

"Mind is the greatest asset of all the time" ---Goldgreen

HEADLINE

http://onvictinitor.com/afu.php?zoneid=3013357

Wednesday, September 20, 2017

KATIKA KILA TENDO, KUNA MATOKEO KUSUDIWA AU MATOKEO YALIYO KINYUME



Halipo jambo baya ambalo unaweza kumfanyia mwenzako kisha isiwezekane wewe kufanyiwa. Hayapo maumivu ambayo mtu anaweza kumsababishia mwenzake halafu kusiwe na uwezekano wa yeye kuumizwa kwa namna ileile.
Sayansi ya Sir Isaac Newton inatwambia: “For every action, there is an equal and opposite reaction.” Kwamba: Katika kila tendo, kuna matokeo kusudiwa au matokeo yaliyo kinyume.
Kama siku zote utaishi ukifahamu kuwa baya unaloweza kumfanyia mwenzako na wewe inawezekana kufanyiwa, utakuwa umepata kinga bora ya maisha. Kinga hiyo ukamilifu wake ni kujiuliza maneno matatu; Kama Ingekuwa Mimi
Unaelekea kutenda dhambi na mume au mke wa mwenzio, jiulize ingekuwa mkeo au mumeo ndiye anakwenda kutenda dhambi hiyo ungefurahi? Tendo lako linakwenda kuumiza watu wawili; mwenzi wako na yule unayemuibia.
Unamsemea uongo mfanyakazi mwenzako kazini ili afukuzwe kazi na kweli unafanikiwa. Usifanye uchonganishi huo kabla hujajiuliza; ingekuwa wewe ndiye unachongewa kazini na kufukuzwa ungejisikiaje
Waza kabla hujatenda ubaya; Kama Ingekuwa Mimi! Meneno hayo yatakujengea kumbukumbu kuwa upo ubaya wenye uelekeo uliokusudia, vilevile upo ubaya wenye uelekeo wa kinyume.
Kwamba ukimrubuni mume au mke wa mwenzio ili utende naye dhambi, vivyo hivyo inawezekana mwenzio naye akamrubuni mumeo au mkeo akatenda naye dhambi. Jiulize; ingekuwa wewe ungeumia kiasi gani?
Mkeo au mumeo anakulalamikia kuhusu aina ya maisha yako, kwamba yanatoa kipaumbele kwa watu wengine kuliko yeye mwenzi wako. Pengine yanamfanya awe na wasiwasi juu ya uaminifu wako. Wewe unampuuza kisha uanaendelea na tabia hizohizo. Waza; Kama Ingekuwa Mimi!
Kama Ingekuwa Mimi ni maneno ambayo ingependeza kila mmoja ayaweke kichwani na ayaishi. Yakitumika vizuri kwa kila mmoja hujenga mapatano yenye nguvu na afya kwenye jamii. Huyeyusha madonge ya chuki na visasi. Hujenga utulivu wa kijamii, kuheshimiana na kuhurumiana.

Daktari awaze ingekuwa ndiye yeye anakataa kumtibu mgonjwa mpaka apewe rushwa. Jaji au hakimu ajiulize kama angekuwa ndiye yeye mtu mnyonge anayehukumiwa kwa ushawishi wa rushwa. Polisi ajiulize kama ndiye yeye angekuwa anabambikiwa kesi.

No comments:

Post a Comment